Sunday, 22 July 2018

Ni Kazi ya Nani..??

Ni Kazi Ya Nani??
Hii  ni hadithi niliyoisikia miaka  kadhaa  iliyopita  kuhusu  watu wanne waitwao Kila mtu, Mtu  fulani,  Mtu  yeyote, na Hapana  Mtu... Kulikuwa na kazi muhimu ya kufanywa na Kila Mtu alikuwa na uhakika  Mtu  fulani angeifanya.  Mtu yeyote  angeliifanya,  lakini Hapana  Mtu aliyeifanya.  Mtu Fulani  akakasirika  kuhusu  hayo kwa sababu ilikuwa kazi  ya  Kila Mtu. Kila Mtu alifikiri  Mtu yeyote angeliifanya,  lakini  Hapana  Mtu aliyetambua kwamba  Kila Mtu hangeliifanya.  Mwishowe,  Kila Mtu alimlaumu Mtu fulani wakati Hapana Mtu aliyefanya kile kile Mtu yeyote angelifanya.

Wakati fulani nilisoma  kuhusu kisa  cha  kushangaza kinachoonyesha mambo muhimu  ya hadithi hii  ya kusikitisha ya ukweli.  Mnamo mwaka  1964 Catherine  Genovese  alidungwa kisu na  kufariki  katika  kipindi  cha  dakika thelathini  na tano  ilhali majirani thelathini na nane wakitazama.  Hatua  waliyochukua ilielezewa  kuwa  baridi na  ya  kutojali,  matokeo  ya  ubaguzi  wa mijini. 


Baadaye, utafiti uliofanywa  na Latane na  Darley ulionyesha kwamba  hakuna  mtu aliyesaidia  kwa  sababu kulikuwa  na  watu wengi walioshuhudia  kwa  kuangalia tu. Watu hao  waliangaliana  ili wapate mwongozo  kuhusu kile wanachopaswa  kufanya.  Kwa  vile hakuna aliyefanya lolote, walibaini kwamba  hakuna anayepaswa kufanya lolote. Watu huenda wasipate  msaada  wakati wanapouhitaji  huku idadi ya  wapita  njia ikiongezeka. 
Mwanafunzi mmoja  aliyekuwa na maradhi ya kifafa alisaidiwa kwa asilimia  85 wakati mpita njia mmoja  alipokuwa  karibu,  lakini wakati watu kadhaa  waliposimama karibu naye na kutazama alipokea msaada wa asilimia 31 pekee.

Ufatifi huu unadhihirisha  kwamba  kadiri watu  wengi zaidi wanapokosa  kufanya  jambo,  watu zaidi hawatafanya  lolote,  bali ikiwa hata  kundi  dogo la watu waliojitolea  litaanza  kuwasaidia watu wengine  kwa kuwatunza na kuwapenda, kutabasamu na kuwakubali,  kuwaheshimu na  kadhalika,  kundi hilo linaweza kukua. Utafiti umethibitisha  kwamba  tunaathiriwa sana na kile  watu walio  karibu nasi hufanya. Tunaangaliana  ili  kupata  mwelekeo hata wakati tusipofahamu kwamba  tunafanya  jambo  hilo. Watu wengi watakubaliana  na maoni ya wengi hata  ikiwa kweli  hawakubaliani na maoni hayo. Hufanya hivyo ili wawe sehemu ya kundi.

Ikiwa tunataka  kuwa sehemu ya Mageuzi ya Upendo, sisi  kama Wakristo  lazima tuwe mfano kwa wengine  badala  ya kujiunga kwenye  mfumo wa ulimwengu. Mtu  fulani  mwenye  ujasiri  wa kutosha  angetokea kuchukua hatua  au kuwa  na upendo  mwingi wa kusaidia, maisha ya  Catherine Genovese yangeokolewa.

No comments:

Post a Comment