Je, umewahi kugundua kwamba Yesu hakuzungumzia shida zake? Angeweza kufanya hivyo; Alikabiliana na mambo yale yale tunayokabiliana nayo mimi na wewe. Yesu alikuwa na ratiba iliyojaa shughuli.
Yesu alikumbana na watu wajeuri na wanaoudhi. Yesu alikabiliana na hali ngumu. Bila kutaja kwamba alifahamu fika kwamba atateseka sana na kufa msalabani kwa ajili ya dhambi za ulimwengu. Lakini ukisoma Injili, hutamsikia Yesu akisema chochote cha kukashifu au kinachoweza kuitwa kulalamika au kunung’unika. Bila shaka alijua nguvu za maneno. Wakati wa mateso na kifo chake ulipokaribia, aliwaambia wanafunzi wake kwamba hatakuwa akiongea nao kwa muda mrefu kuanzia wakati huo na kuendelea (Yohan 14:30).
Kwa nini alisema hivyo? Ilikuwa ni kwa sababu alijua nguvu ya maneno, na pia alijua jinsi ilivyo rahisi kuongea mambo yasiyofaa wakati tunapitia wakati mgumu au wa uchungu. Alijua kwamba Baba yake alikuwa na mpango wa kumwokoa mwanadamu na kwamba mpango huo ulimtegemea yeye, na aliazimia kufanya kila alichotakiwa kufanya ili atekeleze makubaliano aliyokuwa nayo na Mungu, ikiwemo kuongea maneno ambayo Mungu angetumia, si maneno ambayo ibilisi angetumia.
Mimi sitasema nanyi maneno mengi tena, kwa maana anakuja mkuu wa ulimwengu huu, wala hana kitu kwangu. [Hatufanani kwa lololote; hakuna chochote ndani yangu kilicho chake, na hana nguvu juu yangu.] Lakini ulimwengu ujue ya kuwa nampenda Baba; na kama vile Baba alivyoniamuru; ndivyo nifanyavyo. Ondokeni, twendeni zetu.Yohana 14: 30–31
Bila shaka, Yesu alizungumzia mambo mengi, ikiwemo dhambi. Kuna wakati ambapo Yesu aliwakemea Mafarisayo na kuwakosoa wanafunzi wake.
Unaposoma Injili, utaona kwamba Yesu aliongea kuhusu mambo mengi, lakini shida zake hazikuwa miongoni mwa mambo hayo. Luka 4:22 inasema kwamba watu “walistaajabia maneno ya neema yaliyotoka kinywani mwake.” Yesu alikuwa amekuja kutekeleza kazi fulani, na hakutaka kuiacha njia kwa kuangazia matatizo ya kila siku katika maisha Alisema kwamba maneno yake ni roho na tena uzima (Yohana 6:63).
Je, wewe maneno yako ni roho na tena uzima, au ni ya kimwili (kibinadamu) na mauti? Habari njema ni kwamba unaweza kubadilika hivi sasa ikiwa unataka kufanya hivyo. Mimi ndiye mtu wa kwanza kukiri kwamba kinywa ni kiungo ambacho huwezi kukidhibiti bila msaada kutoka kwa Mungu. Hata hivyo, tukifanya uamuzi sahihi na kukubaliana na mapenzi ya Mungu katika sehemu hii, bila shaka atatusaidia kufanya mabadiliko mazuri.
Jimmy J.
Mtumishi.
Mtumishi.
No comments:
Post a Comment