Thursday, 26 July 2018

Matarajio Mapya na Makubwa Zaidi

Tunasema mwanamke mjamzito anatarajia “kujifungua.”  Hivyo huanza kuandaa  mipango  mapema.  Anatenda  sawa  na  matarajio yake—hununua  nguo,  chupa,  kuandaa  chombo  cha  kumlazia mtoto, na kuandaa mahali pa kumweka ili akue.
Tunapaswa kutenda kama watu walio na matarajio. Sharti  tuamke asubuhi na tuandae mipango ili Mungu afanye  kitu cha ajabu. 

Kwa msaada  wa Mungu, tunaweza kuwaza hivi  Huenda leo ndiyo siku. Siku ni hii Bwana  amefanya, na kitu kizuri hakina  budi kutendeka  kwangu .  Hata ikiwa Mungu hatakupa kile kitu ulichokiomba,  jaribu kupanua mtazamo wako. Pengine  unaomba kitu na huku Mungu ana  kitu kingine kizuri  zaidi.  Usiombe  tu  kitu  kizuri;  amini  na  uwe  na  matumaini  ya makubwa zaidi. Amka  kila  siku  na  useme,  “Nina  matarajio  mazuri  na  ya  kwamba  kitu  cha  ajabu  kitatendeka  leo.  


Mke/mume  wangu atanibariki.  Watoto  wangu  watakuwa  na  adabu.  Naenda  kupokea habari nzuri sana kazini. Mungu anaenda  kunipa nafasi ya kumbariki  mtu. Kuna baraka fulani zitakuja kwa  njia ya barua. Leo  naenda  kupata  ushindi.” Usiogope  kuamini,  amini,  na unene  baraka  juu  ya  siku  yako  mara  tu  unapoamka.  Nimeamua kukiita  kitabu  hiki,  “Kitabu  cha  Matumaini mapya, nitakichapa hivi karibuni.”  Ninaamini  kila  mtu atakayekisoma atakuwa  na furaha  zaidi  kushinda  awali.

Matumaini ni kule kuamini kwamba kitu kizuri kiko karibu kutokea! Matumaini huondoa mipaka ya matarajio  yetu.  Je, unatarajia mambo machache  au  mengi  kutoka kwa Bwana? Unaweza  kuwa umefika  katikati  ukitarajia  Mungu  afanye  kitu.  Huenda  umefika katikati  ukiamini kwamba kutatokea  kitu kizuri, lakini nataka kukupa  changamoto  uamini kikamilifu  na kwa moyo wako wote kwamba  makubwa  zaidi  yatatokea  kuliko  awali.

Nataka  kukupa changamoto uamini  kwamba Mungu  anaweza kukutumia  kwa  njia ya ajabu. Ikiwa unatunga nyimbo, kwa nini Mungu asikupe wimbo mzuri  zaidi  kuwahi  kutungwa?  Ukihubiri  Neno,  kwa  nini  Mungu asikupe ujumbe  mzuri, wenye  upako, hivi kwamba kila wakati unapohubiriwa, wafungwa wanawekwa huru? Ikiwa unalea watoto, kwa nini watoto  wako wasije kuwa watu  wanaoleta  mabadiliko makubwa duniani? Kwa  nini usipandishwe  cheo  kazini? Kwa  nini usikutane na mtu yule utakayemuoa au atakayekuoa na kuwa  na maisha  mazuri sana? Kwa nini  usiushinde  uchungu uliosababishwa na watu?  Kwa nini usilete  mabadiliko katika maisha ya watu walio karibu nawe?  

Ni  wakati  wa  kuishi  ukiwa  na  kiwango kipya cha matarajio  yenye matumaini. Amini kwamba ikiwa  kitu kizuri  kinaweza  kutokea kwa mtu yeyote, basi kinaweza  kutokea  kwako!


Jimmy J.

No comments:

Post a Comment