Kushindwa hakutanishinda kamwe mimi ikiwa ari yangu ya kufaulu ina nguvu za kutosha. Og Mandino
Hamu ni motisha yenye nguvu. Imekabiliwa na ukweli kwamba ikiwa kwa kweli nataka kufanya kitu fulani, nitatafuta njia ya kukifanya. Watu mara nyingi huniuliza jinsi ninavyofanya kila kitu ninachokifanya, na mimi husema, “ni kwa sababu nataka iwe hivyo.” Hutambua kwamba Mungu amenipa neema na huweka hamu moyoni mwangu, lakini ni ukweli kwamba nataka nifanye mambo fulani yanayonitia moyo kuyafanya. Ninataka kufanya kile Mungu anachotaka mimi nifanye; ninataka kuwasaidia watu na nataka kutimiza lengo langu, au kama mtume Paulo asemavyo, “Nataka kukamilisha safari yangu.”
Waweza kuuliza, “Je, iwapo sina hamu hiyo?” lazima unayo hamu ya kufanya mapenzi ya Mungu au ungekiweka fundisho hili chini baada ya kusoma mlango wa kwanza. Ikiwa una uhusiano na Mungu kupitia Yesu Kristo, basi una hamu ya kufanya mazuri kwa sababu amekupa Moyo Wake na Roho Yake. Ezekieli 11:19 anaahidi hivi: “nami nitawapa moyo mmoja, nami nitatia roho mpya ndani yao; nami nitauondoa moyo wa kijiwe katika miili yao, nami nitawapa moyo wa nyama; [unaosikia na kujibu unapoguswa na Mungu wao].”
Twaweza kuwa walegevu, tusiotenda lolote, au wachoyo na tunahitaji kukabiliana na maswala hayo wakati mwingine, lakini kama watu wamwaminio Mungu haiwezekani kuwa na moyo wa Mungu na usimwogope na kuwasaidia watu. Nadhani swali ni: Unataka iwe kiasi gani? Je, unataka yakutosha uwache mambo mengine ili upate? Hivi majuzi mwanaume mmoja aliniambia jinsi alivyokosa furaha. Aliendelea kuniambia kwamba anajua Mungu anamuita aje mahala pakuu zaidi lakini anaonelea kwamba hanuii kujitolea inavyohitajika. Nilihisi vibaya kwa ajili yake kwa sababu sitaki akose furaha iliyo upande mwingine wa kujitolea. Ninaomba abadili mawazo yake.
Ikiwa kweli twataka kufanya kitu, tunatafuta njia ya kukifanya. Ni hadi tutakapokubali haya, tutatumia maisha yetu tukidanganywa na vijisababu vyetu kuhusu ni kwa nini hatuwezi kufanya mambo. Visababu ni hatari, na ninaamini ni moja ya sababu kuu zinazotufanya tusiendelee kama tunavyotarajia.
Pengine ungependa kujaribu, lakini unatoa kisababu kuhusu ni kwa nini huwezi. Pengine unataka kuwa na muda zaidi na familia yako, lakini una sababu kuhusu ni kwa nini huwezi. Unaweza kutambua kuwa unahitaji kujitolea zaidi kuwasaidia wengine na ungetaka kufanya hivyo, lakini kila mara kuna sababu (Visababu) ni kwa nini huwezi kufanya. Shetani ndiye anayetupatia visababu; ni hadi tutakapotambua kwamba hali hiyo inatufanya tudanganyike na tusimwogope Mungu, tutakwama katika hali ya kukosa furaha, na kutozaa matunda maishani.
Jimmy J.
No comments:
Post a Comment