Sunday, 29 July 2018

Somo kutoka kwenye Mkahawa

Ninaamini sote  twahitaji  kufikiria makundi ya  kujumuika nayo na kuyapanua.  Twahitaji kuyapanua  vya kutosha ili  kujumuisha watu wa  aina  yote. 

Hivi majuzi nilikuwa na  Rafiki yangu Paul  mwimbaji anayehudumu huko Birmingham, Uingereza, na tulikuwa tukinywa kahawa katika mkahawa mmoja na watu kadhaa. 


Nakumbuka kuangalia  mtindo wa  nywele  wa  msichana  aliyekuwa akitusubiri na kusema kweli,  lilikuwa ni  jambo la kushangaza  ambalo  sijawahi kuona.  Kichwa  chake chote  kilikuwa kimenyolewa  isipokuwa  kwa kile  kiitwacho mtindo wa  ‘Mohawk’ kwenda chini  kati kati, na zilikuwa  na  rangi  nyeusi, samawati,  nyekundu  na nyeupe.  Pia  pua Yake , ulimi  wake, mdomo, sehemu  kadhaa  kwenye masikio yake alikuwa amedungwa. Ninakumbuka kuhisi  vibaya mno  kwa sababu  hakuwa  na chochote  sawa  na  mimi. 

Tulikuwa tofauti  kabisa  hivi kwamba siwezi kufikiria chochote cha kusema kinachohusiana nami. Nilitaka  kuagiza  kahawa  yangu  na  nijaribu kutomwangalia sana.   Paul,  kwa  upande mwingine,  alianza  kuzungumza  naye na jambo  la  kwanza  alilosema  ni, “ninaupenda mtindo wa  nywele zako. Je, unawezaje kuzifanya zisimame  namna hiyo?”  Aliendelea kuzungumza naye  na hali bora ya uhusiano   ambayo haikuwa awali ikaanza  kujidhihirisha. Katika muda mfupi  sote tukawa  huru na ningeweza  kuhisi  sote tunaanza  kuungana  katika mazungumzo  na kumjumuisha katika kundi  letu. 

Nilijifunza  funzo  kubwa siku  hiyo- kwamba  mimi  si  wa “kisasa”  kama ambavyo ningependa kufikiria.  Pengine mimi  ndiye niliyekuwa  tofauti.  Kwanini  twajiweka  sisi kuwa  viwango  kwa kile  kinachokubalika na kudhani  kwamba  mtu yeyote aliye tofauti nasi lazima awe ni  tatizo? Ni  mtindo  upi  wa  nywele  ulio  sawa,  au mtindo wa  nguo? 

Siku moja  nilianza kufikiria kuhusu kile ambacho Musa lazima alikiangalia aliporejea kutoka  kwenye mlima  Sinai, ambako alimaliza  siku  arobaini mchana  na usiku akipokea Amri Kumi  kutoka kwa Mungu. Nina hakika nywele  zake  zilikuwa zimeharibika, ndevu zake zilihitaji kunyolewa,  na nguo yake na viatu zilikuwa chafu.

Ninajua  ya  kwamba  Yohana  Mbatizaji  alikuwa  mtu wa  ajabu. Aliishi  jangwani  peke yake na kuvaa  ngozi za  wanyama  na kula asali  na  nzige.  Wakati alipojitokeza,  alipiga  ukelele  akisema,  Tubuni ninyi wenye dhambi, kwa kuwa Ufalme wa Mungu u karibu!”

Biblia inatufunza kwamba tunapaswa  kuwa  waangalifu  jinsi tunavyowahudumia wageni kwa  sababu huenda tunawakaribisha malaika  bila kujua (angalia EBR 13:2). Inasema tunapaswa  kuwa wakarimu, wenye  uhusiano mzuri,  kuwa na urafiki, na neema  kwao na  kushiriki  starehe  ya  nyumba zetu. 
Watu wengi katika  jamii hivi leo hata hawazungumzi na wageni, mbali na kuwa na urafiki nao. Ninajua, ninajua; pengine  unasema, “Jimmy, tunaishi katika ulimwengu tofauti  hivi leo! Hujui  unayezungumza  naye!” Ninatambua kuwa ni lazima utumie  hekima, lakini  usiruhusu hofu ikufanye usiwe na urafiki na uwe baridi. Kwa kweli  unaweza kumtafuta mtu  mpya kanisani,  mahali pa kazi, shuleni,  au katika mazingara yako na useme jambo!

Kwa  kweli  waweza  kuzungumza na mama  mzee aliyekaa katika ofisi  ya daktari  unaposubiri kuitwa kumuona.  Anaonekana yuko na  upweke; kwanini usimpe  dakika  kumi  za  kuzungumza naye na  uwache  akuambie kuhusu hali yake.  Pengine hutamwona tena,  lakini atakukumbuka.  Aha,  na kweli, Mungu atafurahia  kile ulichomfanyia. Ndio, ni kitu kidogo, lakini ulimjumuisha!

Ikiwa  ufufuo  wa  kweli  utakuja  katika  kanisa  lako, utafurahia kweli  au utaondoka kwa  sababu watu wengi watakuwa  kama  Jamie alivyokuwa  au ni  wabaya  sana? Huenda  watakuja kutoka  kwenye makao  ya muda na wasiwe na harufu  nzuri, au huenda  wananuka pombe na  mambo  mengine yasiyofaa. 

Watu  walioumia duniani kila mara  hawaonekani  wakiwa  katika  hali ya  kupendeza  wala  kuwa na harufu  nzuri. Wakati mwingine  huonekana wakiwa  katika  hali nzuri  lakini  sio kila mara na ni  lazima tukome kuwahukumu  kwa jinsi  tunavyowaona  na  Kuwa tayari kutazama mbele  zaidi  jinsi  watu wanavyoonekana na utafute kujua ni kwanini iwe hivyo.


Jimmy J.

No comments:

Post a Comment