Wednesday, 11 July 2018

Nia Nzuri Haitoshi

Nilisikia  hadithi moja kuhusu  mwanaume mmoja  aliyekwenda nchini  Urusi  akiwa  na nia nzuri  ya kuwaambia  watu kuhusu  upendo wa  Yesu Kristo. Wakati wa  ziara yake, watu wengi walikuwa wanakabiliwa na  njaa.  Alipopata  foleni ya  watu wakisubiri kwa matumaini  ya kupata  mkate wa  siku, aliwafuata  akiwa  ameshika vijikaratasi  vya  habari ya  injili  mkononi na akaanza  kutembea akifuata  foleni  hiyo akiwaambia  kwamba  Yesu  anawapenda na kumpa kila mmoja kijikaratasi  chenye habari ya  ujumbe  wa wokovu. Kwa  kweli, alikuwa  anajaribu kusaidia, lakini mwanamke mmoja akamwangalia  machoni  mwake na akasema  kwa  uchungu, “Maneno  yako ni  matamu, lakini  hayajazi  tumbo langu lililo  tupu.”

Nimejifunza  kwamba  baadhi  ya  watu wanaumia vibaya  mno kusikia habari njema kwamba  Mungu anawapenda,  ni lazima washuhudie upendo huo na  njia moja  bora  ya  jambo  hilo kutendeka ni  kupitia sisi ili  kutimiza  mahitaji yao  kwa  vitendo  na vile  vile kuwaambia kwamba wanapendwa. Ni lazima  tujihadhari  juu ya  kufikiri  kwamba  maneno yanatosha. Yesu vile vile alihubiri kuhusu habari njema, lakini mahali alikokwenda alitenda mema na  kuwaponya  wote  waliopondeka mioyo (angalia MDO 10:38).

Lazima tujihadhari juu ya kufikiri kwamba maneno yanatosha. Kuongea si ghali,  wala  hakuhitaji juhudi  kubwa, lakini  upendo  halisi ni ghali.  Ulimgharimu Mungu Mwanawe wa  pekee na  kuuruhusu upendo halisi kutiririka  kwetu pia  nasi  twahitaji  kugharamika. Pengine  tutahitaji kuwekeza  muda, fedha, juhudi au mali zetu… lakini utatugharimu!
Mungu Anatutegemea Sisi Nitaondoka  nyumbani hivi karibuni kwenda kupata  kikombe cha kahawa  na marafiki zangu na baadaye twende  kwa  chakula  cha mchana.  Pengine  tutatumia muda wa  saa  mbili na wakati huo takribani watoto  240 watakuwa  wametekwa  nyara na kuingizwa katika  sekta  ya ulanguzi wa  kingono. Hii  inamaanisha  kuwa watoto wawili kila dakika  maisha  yao  yataharibiwa  na  mtu aliye mchoyo na mlafi  na ni  hadi pale tutakapofanya jambo.

Twaweza kufanya nini?  Twaweza  kujali, twaweza  kupata  habari, twaweza  kuomba na twaweza  kuchukua hatua. Twaweza  kusaidia huduma  na mashirika yenye  kumbukumbu  zilizothibitishwa  za kuwaokoa  watoto  na wanawake kutokana  na hali hizi za  kutisha,  au ikiwa  Mungu ametupatia  mzigo huo  twaweza  hata  kuchagua  kufanya  kazi  katika maeneo  haya.Ikiwa kazi ya kufanya kila siku  haiwezekani, twaweza kufikiria  kufanya mradi fulani  au kufanya ziara fupi  ya huduma  ya umishenari.

No comments:

Post a Comment