Tuesday, 24 July 2018

Endelea kwenda mbele.

Wanyama  mbalimbali  huwa na silika tofauti  wanapotishwa au wanapokabiliana  na woga.  Kushambuliwa  na dubu, kupandwa na kuchakuro, kushtuliwa  na paa anayekimbia, na fuko  anayechimbua. Muitikio  haya  yote  ya  silika  yanafanya  kazi. 
Lakini  kuna  mdudu mmoja  ambaye  huitikia  kwa  njia  tofauti:huyu ni kifaurongo. 

Kifaurongo  ni mdudu ambaye hamkimbizi mtu, hapandi, hatoroki, au kuchimbua. Kifaurongo hujigandisha tu.  Badala  ya kufanya kitu,  hujigandisha tu.  Hujifanya  amekufa—  ndipo  tunapata  ule  msemo  wa  Kiingereza unaosema  “playing  possum”  (kujifanya  kifaurongo)—na  hutumaini kwamba kwa kujigandisha atakamilisha kitu fulani. 


Nimeona  hilo  mara  nyingi wakati  watu  wanapoumizwa au kutishwa, wanakuwa vifaurongo  wa  kiroho.  Badala  ya  kufanya kitu, wanajigandisha tu. 

Mambo yanapokuwa  magumu, wanapokabiliana na uchungu fulani au kuvunjwa  moyo, wanajigandisha.  Wanaacha  kusonga  mbele.  Je,  hili  ni  jambo mnalolijua?  Je, umewahi kujikuta katika hali ya kutulia  mahali pamoja kwa sababu ya majaribu uliyokuwa huyatarajii  au jambo la kuvunja  moyo sana?

Je, umewahi kuwa katika  hali fulani  ambapo hujui ufanye nini, na hivyo ukaamua kuwa hutafanya kitu? Ikiwa  umekabiliana na uchungu ambao umekugandisha  njiani, basi fahamu kwamba sichukulii uchungu wako kuwa jambo dogo. Kusema  kweli;  nimepitia  mambo  mengi  magumu  ambayo yaliniumiza sana mpaka nikahisi  kana kwamba siwezi kuendelea mbele.
Ninaelewa  yale  unayopitia,  kwa  sababu  mimi  pia  nilihisi nimepoozeshwa  na  shida  fulani.  Lakini  ningependa kukutia  moyo kwamba  katika uchungu unaopitia  wakati mwingine jambo zuri zaidi la kufanya ni kuendelea kwenda mbele. Inawezekana bado huna majibu yote. Huenda  ukashtushwa  na hali  hizo.

Huenda  ukahisi kana kwamba ulimwengu  umepasuka. Lakini katika  hali  hizo  ngumu, ukiendelea kwenda mbele, itakusaidia ili usipoteze matumaini. Huenda hutaweza kuona  mwanga wowote  mbele, lakini ukimtwika  Bwana fadhaa zako  na uamini  kwamba yuko  pamoja nawe katika shida  hii, utagundua  uponyaji kadri unavyotembea  pamoja naye. Hatimaye, si  tu kwamba utaona  mwangaza mbele  yako, mwangaza huo utafukuzia mbali kitu chochote kilicho cha giza maishani mwako. Ninaelewa  kwamba,  kwa  kutegemea  ubaya  wa  hali unayokabiliana  nayo,  kutakuwa  na  siku ambazo  utahisi  kwamba hutaki kufanya kitu chochote. Ukipata hasara kubwa bila shaka  ni jambo la  kawaida kuanza mchakato  wa kuomboleza unaojumuisha hatua  mbalimbali. 

Lakini  kadri  unapotia  mchakato  wa  uponyaji, fahamu kwamba jibu la mwisho  si  kujitenga na kuishi  maisha  ukiwa umelemazwa  na uchungu. Mungu anataka  uendelee  kupiga  hatua ya imani, huku  ukiamini  kwamba atakuvusha  salama kutokana na uchungu huo hadi kwenye kitu kizuri zaidi.
Hatua  za  mtu mwema huimarishwa  na  BWANA...    Ajapojikwaa hataanguka  chini,  Maana  BWANA humshika  mkono na kumtegemeza. Zaburi 37:23-24
Fursa  ya  kumtumaini  Mungu  ni  ya  ajabu  sana.  Huturuhusu kuwa na matumaini wakati  hakuna sababu yoyote  ya kuwa na matumaini.  Wakati  inapoonekana  kana  kwamba  umepoteza, unaweza kumtumaini Mungu aongoze hatua zako.

Nimeongea  na  rafiki  ambaye  amepitia  kipindi  kigumu  cha kupambana  na  saratani.  Amefikia  mwisho  wa  matibabu  sasa  na yuko  tayari  kuanza kuishi  maisha yake ya kawaida tena.  Alisema, “Ninaona  vigumu  kujua  jinsi  ya  kuendelea  mbele  kwa  kuwa maisha  yangu hayatakuwa kama  vile yalivyokuwa awali.”

Pengine haya  ni  mambo  unayoyajua  vizuri.  Huenda  umefiwa  na  mpendwa wako na unashindwa utaishi namna gani bila   mpendwa huyo. Huenda umefukuzwa kazi uliyoifanya kwa miaka na mwenyewe ulikuwa unaona  utafanya  kazi hiyo  hadi ustaaafu.  Utafanya  nini sasa?  Tambua hili hata ingawa hujui  utafanya nini, Mungu  anajua. Atakuongoza katika kila hatua utakayopiga.

Jimmy J.
Mtumishi.

No comments:

Post a Comment