Friday, 27 July 2018

Upendo Wajumuisha, Wala Haubagui

Dada aliyefukuzwa kanisani kwa kuvaa vibaya.
" tunavaa vizuri wakati tunapokuja  kanisani hapa  Holiness  Tabernacle. Hakuna jeans, hakuna viatu vya wazi  kama  champali,  na pia unaweza  kufikiria  kuhusu  mtindo  wa  nywele  ambao  si wa  kuvutia sana.  Unajua, switii, kwamba  Yesu  anatufunza tuwe  wanyenyekevu na sio kujivutia sisi  wenyewe. “Akamwonyesha  Jamie  tabasamu ya kejeli na kurudia kumwambia, “Unakaribishwa wakati wowote"

kiwa utawahukumu watu, huna muda wa kuwapenda. Mama Teresa

Jamie aliingia ndani  ya  kanisa kwenye kona  ya barabara ya  Spruce Avenue  na barabara ya  Twenty-Third huko Harbor, Illinois. Alikuwa akitafuta  msaada.  Alikuwa ameliona jengo la kanisa kwa muda mrefu  na aliwatazama watu wakiingia  na kutoka  mara  mbili au mara  tatu kwa  wiki. Jamie mara  nyingi  alikaa  kwenye mkahawa upande  wa  pili  wa  barabara kutoka  kanisa hilo, akinywa  kikombe cha  kahawa,  akishangaa  jinsi anavyoweza  kukubaliwa  ikiwa atakuwa na moyo wa kuingia  katika moja ya ibada za kanisa.


Jamie alikuwa  katika shule  ya watoto  ya Jumapili  kanisani mara chache  alipokuwa  mtoto  wakati alipohudhuria na jirani mmoja,  lakini alifahamu machache  sana  kuhusu  utaratibu ufaao wa  kuhudhuria kanisa.  Alikuwa hana  hakika  iwapo anafaa  kuingia au atakubaliwa,  kwa  hiyo alikunywa kahawa  yake na kutazama. Alijaribu  kuona ikiwa watu wa kanisa walionekana kuwa na furaha yoyote  walipotoka  nje kuliko  walipoingia,  lakini wote  waliondoka haraka kwa hiyo hakuweza kujua wazi. Mara  kwa  mara  mtu fulani kutoka  kwa  ibada  ya  kanisa  alikuja kwenye mkahawa  baada  ya kanisa. 

Wachache  kati yao  walikaa  peke yao  na  kwa  kweli walionekana  kuwa  na  upweke kama  alivyohisi. Baadhi  yao  walikuja  na  watu  wengine na  walicheka  na  kuonekana kuwa na furaha,  hali iliyompa tumaini  kwamba  huenda  siku  moja akawa na moyo wa kuhudhuria ibada.

Jamie alilelewa  katika familia ambayo haikumjali sana. Wazazi  wake wote walikuwa walevi  na ingawa hawakumdhulumu, walimharibia  sana  kielelezo  chake kwa  kuwa  haraka  kumkashifu na kumtafutia makosa.  Mara nyingi  walimlinganisha na nduguye wa  kiume  aliyeonekana kuwa   mwerevu na mwenye kipawa  kuliko yeye katika  kila njia.  Kila mara  alihisi kuwa  hapendwi,  ana  sura mbaya,  na  ni mjinga,  na  ni kama  hana  thamani    yoyote  hata  kidogo. Alipotimu umri wa  miaka  kumi na  mitatu,  Jamie alikuwa ameangukia  kundi la  watu  wabaya  na  alikuwa  akinywa  pombe na kutumia dawa  za  kulevya. 

Uchungu wa  hisia zake ulikuwa mwingi hivi kwamba  alitumia dawa  za  kulevya  kuutuliza. Pia  alianza  kuwa na  matatizo  ya  kula chakula  kingi kupita  kiasi na  kisha  kukitapika ovyo –hali iitwayo “bulimia.”  Alikuwa  anakula  chakula  kiasi cha kawaida,  kingi mara moja,  lakini  kila mara alijilazimisha kutapika baada ya kula kwa hiyo hangenenepa. Alikuwa  hajasahau  siku ya  kuzaliwa  kwake alipotimu umri wa  miaka  kumi na miwili wakati mama  yake alipomwangalia   kwa hasira na kusema, “Sikuwa na wakati wa kukuokea keki  ya siku  ya kuzaliwa, lakini hata hivyo huihitaji.

Umenenepa  vyakutosha!”  Alikuwa  hajawahi  kufikiria yeye ni mnene  hadi siku hiyo,  lakini kila siku tangu  siku hiyo,  alijiangalia kwenye kioo  na  kuona  msichana  alionekana  kuwa  na  uzani wa pauni thelathini kuliko  alivyokuwa.  Kielelezo  chake kiliharibika kupitia mambo ambayo mama  yake alikuwa  akimwambia  kila mara. Gredi za  Jamie shuleni  hazikuwa  nzuri sana  na  hakuhisi kuwa alikuwa “mwanafunzi wa  chuo,”  kwa  hiyo alipofuzu  kutoka  shule ya upili  alipata  kazi kwenye duka la kuuza bidhaa  za  matumizi ya nyumbani  kwenye  sehemu  hiyo. Hakupata pesa za kutosha za kumwezesha kuondoka nyumbani  kwao  na kuweza  kujitegemea kwa  kuwa na makazi yake mwenyewe, lakini aliweza kununua nguo, uraibu wake wa  pombe,  na  dawa  zake za  kulevya  wakati alipotaka kujistarehesha.  Wakati wake mwingi wa  kupumzika aliepuka kuwa  nyumbani kwa  kukaa  katika  mkahawa  au kutembea hapo karibu na  kwao  na  akashangaa  jinsi familia nyingine  zote  zilizoishi hapo  zilivyokuwa. 

Hakuwa  na  marafiki wa  kweli-watu anaoweza kuwaamini na  kumhesabu kuwa  yeye yupo.  Watu waliokuwa katika  maisha  yake walikuwa  watumiaji, wala  sio watoaji,  na  wengi aliwaogopa. Siku moja hatimaye alijihisi kuwa mwerevu vyakutosha kuingia ndani ya  kanisa  ilhali watu wengine  walikuwa  wamekusanyika ndani. Aliingia kwenye umati, akitumai kuwa hangetambuliwa, lakini  akiwa  na hamu ya  kupata mtu  wa kumkaribisha na kusema, “Tuna furahi kuwa nawe siku  ya leo.”  Aliwatambua watu waliokuwa wakimwangalia  na  baadhi  yao  walikuwa  wakinong’onezana,  lakini hakuna  mtu aliyeonekana  kuwa  na  urafiki.  Jamie  alikuwa  amevaa visivyo kwa  mavazi  yanayopendwa  na watu wengi na nywele  zake  zilikuwa na karibu rangi  tatu tofauti.  Zilikuwa  nyeusi,  zikiwa  zina rangi  nyekundu   na rangi  ya  dhahabu. Alikuwa  amevaa  jeans kubwa na shati kubwa.  Hakufanya hivyo kwa kupenda;   alikuwa akijaribu kuficha  kile alichofikiria  kuwa  mwili wake mkubwa.  Alikuwa amevaa  viatu vya  wazi  vya  ngozi sawa  na champali,  ambavyo hakuna mtu aliyekuwa amevaa kanisani-hasa katika kanisa hilo! Jamie alikaa  kwenye mstari wa  mwisho na hakuelewa  chochote kilichokuwa  kikiendelea. Watu walikuwa  mara  wakisimama  na kusoma  mambo  kwenye kitabu kilichowekwa  vizuri kwenye kiti kirefu  cha  kanisani mbele  yao;  kisha walikaa  tena. 

Watu waliimba, kinanda kuchezwa  na maombi na sahani la kukusanyia pesa lilipitishwa karibu na  baadhi  ya  watu wakaweka  pesa  ndani yake. Mwanaume mmoja ambaye hakuonekana  kuwa  mwenye furaha na amekasirika  kidogo alitoa  mahubiri  ya  dakika  ishirini,  ambayo hakuyaelewa  kabisa.  Alifikiri kuwa  alikuwa  kasisi,  lakini hakuwa na  uhakika. 

Hatimaye,  ibada  ilionekana kumalizika kwa  sababu wote walisimama tena na kuimba wimbo mmoja zaidi. Alifikiri pengine  mtu fulani angesema  kitu kwake walipoondoka.  Kwa kweli,  mtu angesema kitu  fulani!  Kasisi alisimama mlangoni akiwasalimia  watu kwa  mkono walipokuwa wakiondoka  kanisani na wakati Jamie alipomfikia hakutabasamu wala  hata  kumwangalia macho kwa macho. Alielewa kuwa anafanya kazi yake na hangelisubiri imalizike. Alipokuwa akiteremka kwenye  ngazi, akatambua kuwa mwanamke mmoja anaonekana anamsubiri yeye hapo chini mwisho wa  ngazi.  Alihisi kuwa  na  furaha  ya  mshangao  akifikiria kuwa  mtu fulani amemtambua  hatimaye.  Mwanamke huyo  alimtambua  ndiyo, lakini alitambua kila kitu alichofikiria  kuwa  makosa  kuhusu  vile Jamie alivyoonekana,  kwa hiyo akasema,  “Jina langu ni  Margaret Brown. Je, wewe  unaitwa  nani?  Jamie  alijibu  kwa  kusema  jina lake na Margaret   akaendelea kusema, “Unakaribishwa  kila mara  hapa, lakini nilifikiri nitakusaidia kwa  kukufahamisha kwamba  tunavaa vizuri wakati tunapokuja  kanisani hapa  Holiness  Tabernacle. Hakuna jeans, hakuna viatu vya wazi  kama  champali,  na pia unaweza  kufikiria  kuhusu  mtindo  wa  nywele  ambao  si wa  kuvutia sana.  Unajua, switii, kwamba  Yesu  anatufunza tuwe  wanyenyekevu na sio kujivutia sisi  wenyewe. “Akamwonyesha  Jamie  tabasamu ya kejeli na kurudia kumwambia, “Unakaribishwa wakati wowote.” Jamie hakuweza  kwenda kwenye mkahawa  siku  hiyo; ilibidi aende mahali pengine na kuwa  peke yake ili alie. Alihisi kwamba sasa  Mungu amemkataa  pia,  na  alimaliza  siku iliyosalia  akiwaza juu  ya  kujiua.  Alikuwa amefika  mwisho chini ya shimo na alihisi kuwa hana sababu hata kidogo ya kuendelea kuishi. Majina haya  yamewekwa.  Lakini ulimwengu umejaa akina Jamie na makanisa  ya  Holiness  Tabernacle na wanawake wa kidini  kama  Bi.  Brown.  Kumejaa  Wakristo  wanaoingia  na  kutoka makanisani kila wiki.

Wengi wao  huenda  na hawawezi kuvumilia hadi ibada imalizike.  Ni watu wa  kupinga,  kuhukumu, na wabaguzi sana! Mungu Anampenda kila mmoja kwa Usawa Yesu pengine hakuwa  katika  kanisa  la  Holiness  Tabernacle  siku ambayo Jamie alikwenda  kwa  sababu hangefurahia  pia.  Lakini angelikuwa huko, angeliwatazama  akina Jamie waliokuja  siku hiyo. Angelikaa  kando yake au kutembea karibu naye hadi mbele ili  kukaa naye, na angeliuliza ikiwa ni  mgeni.  

Angelimweleza kila kitu asichokielewa.  Angelitabasamu mbele  yake kila mara alipomwangalia  na,  kumjua, angelimpongeza  kwa  mtindo wake wa kipekee  wa nywele  kwa  sababu  Yeye  hupenda  aina mbali mbali! Angelimwalika  avuke upande wa  pili wa  barabara  ili kunywa kikombe cha  kahawa  pamoja naye na kundi  alilokwenda  nalo kama kawaida na wakati Jamie alipoondoka angelitarajia kurudi  tena juma lijalo.  Lakini Yesu hakuwako  siku hiyo  kwa  sababu hakuna aliyetenda kama  vile  angetenda.  Hakuna aliyemwakilisha  vyema; na hakuna aliyemuiga Mungu.

No comments:

Post a Comment