Monday, 16 July 2018

Kumjua Mtu Mpya Aliye Ndani Yako.

"Wanawake  wengi  walioolewa  wanajua  kwamba  kubadilisha jina kunahitaji mazoea.  Ulikuwa unaitwa Yasinta Makokoto, lakini sasa unaitwa Yasinta Mapunda. Ulikuwa waitwa  Sally Edward, lakini sasa  unaitwa  Sally Joseph.  Inachukua  muda kuweza kuzoea jina jipya, lakini kumbuka, Paulo alikuwa anakabiliana na tatizo lililokuwa  zaidi  ya  mabadiliko  ya  jina—  Paulo  alikuwa  anapokea mabadiliko  ya  moyo  na  pia  asili. " -Nukuu

Lakini  sisi  sote, kwa uso usiotiwa  utaji, tukiurudisha  utukufu  wa Bwana,  kama  vile  katika  kioo,  tunabadilishwa  tufanane  na mfano uo huo,  toka  utukufu  hata  utukufu, kama  vile  kwa  utukufu  utokao kwa Bwana, aliye Roho. 2 Wakorintho 3:1


“Kuna  mambo  matatu  ambayo  ni  magumu  sana: chuma, almasi, na kujitambua mwenyewe.” —Jimmy J

Mabadiliko  si  rahisi—hata  mabadiliko  mazuri  yanagharimu mazoea. Mungu  anapotubadilisha, huchukua muda ndipo tukaweza  kuamini  kabisa kwamba kweli  tumebadilika.  Mtume Paulo alilifahamu hilo kuwa kweli. Tunapomfikiria  Paulo,  tunapata  mtu  aliyekuwa  na  imani kubwa  sana, mwandishi wa sehemu kubwa  ya Agano Jipya.
Mtu anaposimama  kanisani  na kusema,  “Hebu natusome yale aliyosema  Paulo  katika  Warumi,”  au  “Kama  alivyosema  Paulo katika  kitabu  cha  Wagalatia...”  hakuna  anayepinga.  Lakini  kuna wakati  Paulo  alikuwa  mtu  aliyeshukiwa na  kila  mtu.  Hakuwa mtume  mkuu  kabisa;  alikuwa  ni  mwanadamu  tu  mwenye  jina jipya  na  sifa  mbaya:  Alikuwa  Farisayo  wa  Mafarisayo.  Alikuwa  mtesi wa  kanisa  la  kwanza.

Mtu asiyeweza  kuaminiwa.  Kwa hiyo nashangaa ikiwa  kulikuwa  marekebisho—wakati  ambapo  Paulo  alihisi  yeye  ni Sauli  zaidi  kuliko  Paulo.  Nashangaa  ikiwa  ilimchukua  Paulo  muda kumwacha  Sauli. Nashangaa  ikiwa  alimsalimia  mtu  kwa  mkono na  kusema,  “Habari  gani.  Naitwa  Sauli...  er...um...Yaani,  Paulo. Naitwa Paulo.”
Wanawake  wengi  walioolewa  wanajua  kwamba  kubadilisha jina kunahitaji mazoea.  Ulikuwa unaitwa Yasinta Makokoto, lakini sasa unaitwa Yasinta Mapunda. Ulikuwa waitwa  Sally Edward, lakini sasa  unaitwa  Sally Joseph.  Inachukua  muda kuweza kuzoea jina jipya, lakini kumbuka, Paulo alikuwa anakabiliana na tatizo lililokuwa  zaidi  ya  mabadiliko  ya  jina—  Paulo  alikuwa  anapokea mabadiliko  ya  moyo  na  pia  asili. 

Hebu  mfikirie  akisema  “Habari gani.  Naitwa  Paulo. Sasa  mimi ni mfuasi  wa  Yesu. Ningependa  kukwambia habari  zake.”  Lazima  watu  walimtazama  huyu  mtesi  wa  WakristoFarisayo-aliyegeuka  na  kuwa  mhubiri  na  kujisemea  Ngoja kidogo. Huyu ndiye yule jamaa  aitwaye Sauli.  Nimesikia  habari  zake. Yeye huwakamata na kuwatesa Wakristo... Simwamini na naona vigumu kuamini ikiwa kweli amebadilika! Hata  ingawa tunaweza kubahatisha jinsi  watu  mtaani walivyouchukulia utambulisho mpya  wa Paulo, Biblia  inatwambia namna  wanafunzi  walivyochukulia  jambo  hilo—hawakukubali. 

Hawakushawishika  kwamba  Paulo alikuwa mtu mpya. Matendo 9:26  inasema:  “Na  Sauli  alipofika  Yerusalemu,  alijaribu  kujiunga na  wanafunzi, nao  walikuwa wakimwogopa  wote,  wasisadiki  ya kuwa  yeye  ni  mwanafunzi.”  Ni  kwa  sababu  tu  Barnaba  alisimama mbele  ya wanafunzi na alitetea  tabia  ya Paulo  ndipo wakakubali kumpokea. 
Bila shaka,  tunajua kwamba  hatimaye  walimpokea, na sehemu  ya  hadithi  iliyosalia  ni  historia  ya  Biblia.  Lakini  kuna  kirai kimoja  katika  kifungu  kilichotangulia  ninachotaka  kuwaonyesha: “Wasisadiki ya kuwa yeye ni mwanafunzi.” Kitu cha pekee ambacho kingefanya  kirai  hicho  kiwe  kibaya  zaidi  ni  kama  kingesema:  Paulo hakuamini kwamba kweli alikuwa ni mwanafunzi. Unajua, Paulo hangeweza kudhibiti yale  waliyowaza wanafunzi. Ilibidi Barnaba aongee  na wanafunzi, na ilibidi Mungu aibadilishe mioyo yao. Hayo ni mambo ambayo hayakuwa chini ya uwezo wa Paulo.

Kitu  cha pekee  ambacho aliweza  kukidhibiti  ni mtazamo . Ukweli  usemwe, yamkini haikujalisha watu  walikuwa wanaamini nini. Kilichokuwa muhimu ni kile  alichoamini  Paulo. Kama hangekubali  vile alivyo mtu mpya ndani ya Kristo, basi hangeweza  kuifikia  hatima  yake  maishani. 

Hebu  fikiria  Paulo anatembea  mitaani huku  akijisemea  Natamani  ningeweza  kusafiri  na kulihubiri Neno la Mungu. Hilo  ndilo  jambo  la  kutenda lililo  moyoni mwangu. Lakini nilikuwa mtesi wa  kanisa.  Nitakuwa  Sauli  wakati  wote.  Au  kama  angefikiria  Nilianza maisha  yangu kuchelewa.  Hakuna vile ninaweza kufanya mambo  yote niliyotamani  kumfanyia  Mungu. Nilikuwa  Sauli  kwa  muda  mrefu. 

Kama huo ungelikuwa  ndio mtazamo  wake, Paulo  angekuwa  mtu  wa kusikitisha, na hangetimiza yote aliyopangiwa na Mungu. Lakini  Mungu  alipoanza  kufanya  kazi  maishani  mwake,  Paulo alielewa  kwamba hakuwa Sauli  tena,  kwa  hiyo akaacha kuishi kama  Sauli.  Hakufikiria  tena  kama  Farisayo,  hakuongea  tena  kama Farisayo,  au  kutenda  kama  Farisayo.  Mambo  yalikuwa  tofauti sasa. 

Alikuwa  amebadilishwa.  Alikuwa  amepewa  matumaini.  Na akachagua kuishi hivyo. Ni Paulo, ambaye kwa pumzi ya Roho Mtakatifu, aliandika: Hata  imekuwa,  mtu akiwa  [ameunganishwa]  ndani  ya  Kristo (Masihi)  amekuwa kiumbe kipya  (kabisa);  ya  kale [ile hali ya  zamani  ya  kiroho  na kimaadili]  yamepita,  tazama! Yamekuwa mapya! 2 Wakorintho 5:17 (imeongezwa msisitizo) Kwa  sababu kutahiriwa  [sasa]  si  kitu,  wala  kutotahiriwa, ila [tu] kiumbe kipya [ambayo ni matokeo ya kuzaliwa mara ya pili na asili mpya katika Kristo Yesu, Masihi]. Wagalatia 6:15 (imeongezwa msisitizo) Paulo  alijaa  matumaini,  na alisisimka  juu ya  maisha yake  kwa sababu  “mapya  kabisa”  yalikuwa  yamemfikia—sasa  alikuwa  na asili  mpya  katika  Kristo  Yesu.” 

Paulo  hakutembea  tena  huku akiwaza, kuongea,  kuwa na wasiwai,  akifanya kazi, na kutenda kama Sauli.  Alikuwa amebadilishwa. Paulo  alipokea  mambo mapya  ambayo Mungu alikuwa anafanya  katika  maisha yake, fursa mpya zilizokuwa mbele  yake, na yule mtu mpya ambaye Mungu alikuwa amepanga awe.

No comments:

Post a Comment